Sunday 24 September 2017

MUIGE MARAGA.

Jasmini kipenzi changu, waraka huu Ni wako

Chenille mwana wa kwangu, nisikize mi ninako

Maisha haya ya tangu, jadi zile za Obakoo

 Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.



Ndiye jaji wetu Kenya, Yule mwenye historia

Kazi nzuri alifanya, kila mja kasifia

Wale wezi wa kunyonya, Kura zetu kaangazia

Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.



Nina mengi ya kusema, ila nianzie wapi?

Viongozi waso wema, ila tutaenda wapi?

Nchi yetu uhasama, jamani twaelekeapi?

Mwanagu unapokua, na umuige Maraga



Mwana pendo na Moraa, kafa kisa uchaguzi

Mapolisi kwa vifaa, wakaleta uchafuzi

Wakenya bila manufaa, twasubiri uchunguzi

Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.



Adhis, Nyash na Kadima, wenye wana Kama
mie
Sisi sote kina mama, wenye wana tuangazie

Kuwalea hima hima, kesha kua wajulie

Ili wanapokua, na wamuige Maraga.


Kadi tama Sina budi, mwisho wangu wa waraka

Mwana uwe mwenye udi, nami naomba baraka

Zidi kuwa na juhudi, maisha siwe dhihaka

Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.


Jaji mkuu wa Kenya, David Maraga.

2 comments:

LULU HASSAN

Siulize Ni kwa Nini, Nam enzi huyu Lulu Ueledi wake Shani, taka iga nifaulu Kwenye lugha namba wani, uliza hadi ikulu Mwanahabari shupavu...