Chenille mwana wa kwangu, nisikize mi ninako
Maisha haya ya tangu, jadi zile za Obakoo
Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.
Ndiye jaji wetu Kenya, Yule mwenye historia
Kazi nzuri alifanya, kila mja kasifia
Wale wezi wa kunyonya, Kura zetu kaangazia
Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.
Nina mengi ya kusema, ila nianzie wapi?
Viongozi waso wema, ila tutaenda wapi?
Nchi yetu uhasama, jamani twaelekeapi?
Mwanagu unapokua, na umuige Maraga
Mwana pendo na Moraa, kafa kisa uchaguzi
Mapolisi kwa vifaa, wakaleta uchafuzi
Wakenya bila manufaa, twasubiri uchunguzi
Mwanangu unapokua, na umuige Maraga.
Adhis, Nyash na Kadima, wenye wana Kama
mie
Sisi sote kina mama, wenye wana tuangazie
Kuwalea hima hima, kesha kua wajulie
Ili wanapokua, na wamuige Maraga.
Kadi tama Sina budi, mwisho wangu wa waraka
Mwana uwe mwenye udi, nami naomba baraka
Zidi kuwa na juhudi, maisha siwe dhihaka
Nice piece dear keep it up
ReplyDeleteAsante sana
Delete