Wednesday 31 January 2018

KARIBU DUNIANI

Kupitia somo la kisayansi la Bayolojia, tunaelewa fika kuwa, pindi tu yai la mume linapokutana na yai la mke, iwe ni wakati wa kitendo cha ndoa au la, basi hapo ndipo maisha ya kiumbe chochote kile chenye uhai huanza. Binadamu ni kiumbe ambaye maisha yake ni ya dhamana mno, lakini ukweli ni kuwa wengi wetu tuko hapa duniani kupitia neema ya Mwenyezi Mungu, kwani wana wengi hukufu kabla au hata wakati wa kuzaliwa, sababu zikiwa ni chungu furika.


Lusaka, Zambia. Very pregnant young African woman in ragged clothes outside her poor house on the outskirts of the - Stock Image
 binti mdogo mjamzito
kimedhaminiwa na google
 Uja uzito ni hali ambayo hukumbwa na hali ya sintofahamu na mabadiliko mengi ya kimaumbile. Habari ya kuwa mama mtarajiwa hupokelewa katika hali tofauti tofauti kulingana na jinsi mtu alivyojipanga au hali yake ya maisha. Katika karne ya saa, tunao mabinti wengi ambao hupachikwa mimba wakiwa bado katika umri mdogo. Je, ni vipi mabinti hawa hukidhi hali hii? Wengi wao hulazimika kuavya huku wachache wanao stahimili wakati huu mgumu, hujifungua kupitia shida nyingi ajabu. Safari ya kukaribishwa duniani, je, atafika akiwa hai au maiti? Atafika katika hali ya raha au shida? Atazaliwa hospitalini au atatupwa chooni?

Maisha ya ufukura imesababishia vifo vya watoto wengi kabla ya kuzaliwa au hata wakati au baada ya kuzaliwa. Hata ingawa maisha ya wanawake wajawazito imezidi kuboreshwa, kupitia uanzilishi wa 'Linda Mama Boresha Jamii," inayotoa huduma za bure kwa kina mama waja wazito katika hospitali  za serikali, huduma hizi hazisaidii aslilimia mia ya wanawake. Suluhisho la asilimia mia ni lipi? sidhani nina jibu, ila nawasikitia kina mama ambao wanakumbana na shida hizi, kwani wengi pia hupoteza maisha yao hasa wakati wa kujifungua.

Iwapo wewe ni mzaliwa wa jijini, shukuru Mungu. Iwapo eneo lenu au hata bara kwenu kuna hospitali, na huduma zinapatikana kwa urahisi, basi wewe ni mmoja wapo wa wale wenye bahati nasibu. Tunao adinasi wengi wanaoishi katika maeneo ya kusikitisha sana. baadhi ya maeneo haya ni kama vile sehemu nyingi za kaskazini mashariki. Eneo hizi zina hospitali chache sana za serikali na barabara pia ni duni ajabu, hivyo kuwasababishia wanaoishi mbali kushindwa kufika hospitalini ili kupata matibabu. Je, tatizo hili laweza kutatuliwa na nani kama si serikali? Ahadi tunazo, lakini ngoja ngoja itazidi kutuumiza matumbo, huku watoto wengi wakikaribishwa duniani na kifo.

Mama mja mzito anapaswa kuenda hospitalini takriban kila mwezi ili kuangaliwa iwapo kitoto chake tumboni kinakua salama salimini, au iwapo ana ugonjwa wowote ili kuelekezwa ipasavyo. Katika maeneo ambayo hospitali ni chache na kuna ugumu wa kuyatembelea kutokana na umbali na barabara mbovu, wanawake wengi huamua kuwatembelea wakunga wenye ujuzi ili wasaidike. Wakunga hawa hutumia miti shamba kutokana na itikadi zao za kitamaduni. Mbinu hizi huhatarisha maisha ya mama pamoja na kitoto chake tumboni na hivyo huchangia pakubwa katika vifo vya mama wajawazito au watoto wachanga. Na hivi ndivyo wanavyo karibishwa duniani baadhi ya wana wetu.


Pregnant african woman with child, Madagascar - Stock Image  
mama mjamzito katika eneo duni.
kimedhaminiwa na google



Hiki ni kilio, hiki ni kilio changu na natumai pia ya wale wenye macho ya kuweza kuyaona niyaonayo mimi. kwenye mizani, sijui waweza kuipa serikali uzito upi katika kuangalia maslahi ya kina mama waja wazito, hasa katika haya maeneo duni yaliyojaa walala hoi, wale tuwaitao 'maskini hohehahe.' ? 

Sote ni waathiriwa kwa njia moja au nyingine, kina mama hawa ni jamaa zetu. Sio tu katika maeneo haya, bali nchi nzima inakumbana na shida nyingi katika kuwahudumia kina mama wajawazito. Ufisadi uongozini umekithiri mipaka na kuzorotesha utoaji huduma. Leo hii, idadi ya kina mama katika wadi za kujifungua imeongezeka maradufu, ilhali vifaa ni vile vile(vichache mno). Dawa hazipatikani hospitalini na mara nyingi wagonjwa hulazima kununua dawa katika maduka ya dawa ambayo sana sana zinamilkiwa na wahudumu wa hospitalini, hasa madaktari wenye vyeo kubwa kubwa. Ndiyo huduma ya bure hii, au vipi?


Heko kina mama wote! nawavulieni kofia kwa mengi magumu mliyoyapitia ili kuwafikisha wana duniani. bila shaka tumeijaza alivyoamuru Mwenyezi Mungu. Shukuru ulivyopokelewa duniani, maana ni wengi dunia hii waliionea paa!


Image result for pictures of poor facilities of giving birth in africa
karibu duniani.
kimedhaminiwa na google.

LULU HASSAN

Siulize Ni kwa Nini, Nam enzi huyu Lulu Ueledi wake Shani, taka iga nifaulu Kwenye lugha namba wani, uliza hadi ikulu Mwanahabari shupavu...